Pigo la Mvua ya mawe na Toba ya Farao
26 Ni katika nchi ya Gosheni tu, ambako wana wa Israeli walikuwa, hapakuwa na mvua ya mawe. 27 Ndipo Farao akatuma watu kuwaita Musa na Haruni, akawaambia, Nimekosa wakati huu; Bwana ndiye mwenye haki, nami na watu wangu ndio tulio waovu. 28 Mwombeni Bwana, kwa maana yatosha, ili kuwe na ukomo wa ngururu na mvua; nami nitawaacha mwende zenu, wala hamtakwenda mbali zaidi. 29 Musa akamwambia, Mara nitakapotoka mjini, nitatandaza mikono yangu kwa Bwana; na ngurumo zitakoma, wala hapana mvua tena; upate kujua ya kuwa dunia ni ya Bwana. 30 Lakini mimi najua ya kuwa wewe na watumishi wako hamtamcha Bwana Mungu bado. 31 Na kitani na shayiri zikaharibiwa; maana shayiri ilikuwa imechujwa, na kitani ilikuwa imechujwa.

Elizabeth